Tatizo la Unene Uliopitiliza (Obesity)
Tatizo hili la unene uliopitiliza kuliko inavyohitajika kiafya huwa linaletwa na kuongezeka kwa kiwango cha mafuta mwilini. Njia rahisi na inayokubalika ya kuweza kugundua kama mtu ni mnene kupita kiasi (obese) inafahamika kama kipimo cha Body Mass Index (BMI). Vipimo hivi vya BMI ndio vinaweza kukujulisha kama unene ulionao unastahili kulingana na umri, urefu na uzito wako. Vipimo hivi ni kama ifuatavyo:
Jinsi ya kupima BMI yako
Kanuni ya BMI hutumia uzito wa mtu pamoja na urefu wake. Uzito wa mtu hupimwa katika kilograms (kg) na urefu wake katika mita (m) au sentimita (cm). Ikumbukwe pia kuwa mita moja ni sawa na sentimita 100 na mita² = mita x mita.
| Category | BMI range – kg/m2 |
| Emaciation | less than 14.9 |
| Underweight | from 15 to 18.4 |
| Normal | from 18.5 to 22.9 |
| Overweight | from 23 to 27.5 |
| Obese | from 27.6 to 40 |
| Morbidly Obese | greater than 40 |
BMI (kg/m2) = Uzito katika kilograms/Urefu katika meters². Maana yake ni kwamba ili kuweza kupata BMI itakayokuwezesha kujifahamu kama u mnene ama la, chukua uzito wako gawa kwa kipeo cha pili cha urefu wako.
Tatizo la unene uliopitiliza husababishwa na nini ?
Kuna mambo kadhaa yanayoweza kusababisha unene uliopitiliza. Mambo hayo ni pamoja na
- Vyakula vya mafuta - Ulaji wa vyakula venye mafuta mengi au calories nyingi.
- Kutofanya mazoezi - Wale wasiofanya mazoezi mara kwa mara huwa wanene tofauti na wale wanaofanya mazoezi.
- Kurithi viashiria vya asili (genes) - Viashiria hivi vinaweza kuwa moja ya vichocheo vya kuongeza uzito kwani ndivyo huamua wapi mafuta huhifadhiwa mwilini na kwa kiwango gani. Lakini haimanishi kuwa mtu akiwa navyo basi ndio atakumbwa na tatizo hili.
- Umri - Watu wengi huongezeka uzito au hunenepa kadri umri unavyoongezeka kwa sababu wanakuwa hawajishughulishi sana (less active) na huwa wanapungua maumbile ya miili yao (muscles mass)
- Matatizo ya kisaikolojia - Wakati mwengine watu wenye matatizo ya kisaikolojia au msongo wa mawazo (stress) huwa na tabia ya kula sana, matokeo yake ni kunenepa.
- Dawa - Baadhi ya dawa zenye madhara ya kuongeza unene ni kama corticosteroids, blood pressure medications, tricyclic medications na kadhalika.
- Matatizo ya afya - Baadhi ya magonjwa yanachangia kuongezeka kwa uzito au kenenepa kama cushings syndrome, hypothyroidism, osteoarthritis na kadhalika
Vihatarishi vya tatizo la unene wa kupitiliza

Aidha yapo mambo kadhaa ambayo yanaweza kumuhatarisha mtu kupata unene wa kupitiliza. Mambo haya ni pamoja na
- Kukua kwa uchumi wa nchi - Wananchi wengi wanaoishi kwenye nchi zilizoendelea au wenye kipato kikubwa ndio wanaopata tatizo hili kutokana na kuishi mfumo wa maisha ya kivivu na hali ya kutokufanya mazoezi (sedentary lifestyle).
- Historia ya kuongezeka uzito uliopitiliza kwenye familia nayo yaweza kuhatarisha mtu kupata tatizo hili. Aidha, si jambo la kushangaza kuona karibu familia nzima au wengi wa wanafamilia kuwa wanene kupitiliza.
- Kutojishughulisha na chochote (inactive).
- Kupenda kula sana kuliko kawaida (overeating).
- Kula vyakula vya mafuta mengi
- Kutumia dawa zenye madhara ya kuongeza uzito uliopitiliza.
- Kuwa na ugonjwa wa vichocheo mwilini (hormonal disorders) kama cushing syndrome, hypothyroidism.
- Kuwa na msongo wa mawazo au kuathirika kisaikolojia.
Magonjwa yanaoweza kuambatana na tatizo la unene uliopitiliza
- Kisukari
- Shinikizo la damu (hypertension)
- Kiharusi (Stroke)
- Magonjwa ya moyo
- Tatizo la kutopumua vizuri wakati mtu yupo usingizini (Sleep apnea)
- Vijiwe katika mfuko wa nyongo (Gallstones)
- Kiwango cha juu cha lijamu kwenye damu (cholesterol ikiwemo triglycerides)
- Ugonjwa wa mifupa kama yabisi (osteoarthritis).
- Saratani ya matiti
- Saratani ya tezi dume (prostate cancer)
- Saratani ya utumbo mpana pamoja na maeneo ya haja kubwa (Colorectal cancer)
- Matatizo ya mzunguko na mishipa ya damu kama vile kuvimba kwa vena za miguuni (varicose veins)
Tiba ya kuongezeka unene kupita kiasi
Tiba ya tatizo hili ni mhusika kujitambua ya kwamba ana tatizo na kuwa tayari kupunguza uzito. Mabadiliko ya tabia ya mhusika ni muhimu sana, mabidiliko haya yawe ndio mfumo wa maisha yake ya kila siku.
Kupungua uzito na kujilinda au kutunza uzito ulionao baada ya kupunguza uzito ni jambo la msingi sana na inahusisha mazoezi, chakula na madiliko ya tabia ya mtu.
- Mabadiliko ya tabia - Hii inahusisha muhusika kupunguza kiwango cha chakula anachokula lakini kiwe chenye virutubisho vyote muhimu vya afya na kuongeza kiwango cha ufanyaji mazoezi.
- Mazoezi - Mazoezi husaidia kupunguza uzito hasa kipindi cha miezi sita ya mwanzo na hutunza uzito uliokusudiwa kwa muda mrefu. Pia hupunguza mafuta ya mwilini, huongeza ufanisi wa moyo, hupunguza tatizo la shinikizo la damu (hypertension), na kuweka sukari katika kiwango kinachohitajika mwilini.
Kama hujazoea kufanya mazoezi ni vizuri uanze taratibu na ujiwekee lengo kwa kufanya mazoezi kwa muda wa nusu saa kila siku, siku tano kwa wiki,(dakika 30 kila siku kwa siku tano kwa wiki). Mazoezi mazuri ni kama kuogelea, kuendesha baiskeli, kutembea, kunyanyua vitu vizito (visiwe vyenye uzito mkubwa), mazoezi ya viungo na kadhalika. Kama mtu ni mnene sana basi ni bora kuzungumza na daktari wako kabla ya kuanza mazoezi mapya. Baada ya kuanza mazoezi kwa mara ya kwanza, mwili utakuwa na maumivu, hii ni kawaida lakini kama mtu atapata maumivu zaidi ya masaa 2 baada ya kufanya mazoezi ni vizuri kumuona daktari.
- Dawa - Zipo dawa nyingi za kupunguza uzito lakini ikumbukwe ya kwamba hakuna tiba ya tatizo hili na dawa hizi zina madhara mengi kama kuongeza shinikizo la damu (hypertension), matatizo ya moyo, kuharisha,msongo wa mawazo (depression) na mengineyo.
- Chakula - Msingi wa kupunguza uzito au unene ni kujua ni kiwango gani cha calories mwili wako unahitaji kwa siku ili uwe unakula chakula ambacho hakitazidisha au kupunguza kiwango cha calories unazohitaji kwa siku. Mlo mzuri ni ule ulio na matunda kwa wingi, mboga za majani, nafaka ambazo hazijakobolewa, mafuta kidogo (less saturated fat). Vyakula vengine ni kama mayai, nyama isiokuwa ya mafuta (lean meat), samaki, kuku na vingineyo.
- Tiba ya upasuaji - Kuna aina nyingi za upasuaji ambao unasaidia kupunguza uzito aina hizi ni kama gastric banding, gastric bypass (Roux-en-Y-procedure), liposuction. Kabla ya kufanyiwa upasuaji, muhusika atahitaji kupimwa kisaikolojia (psychological testing) na kupewa ushauri nasaha kwani tiba hii pia ina madhara yake.
Wanawake ambao wana uzito wa kupitiliza (obese women) wakiwa wajawazito wako kwenye hatari ya kupata madhara yafuatayo
- Kisukari cha mimba (Gestatitional diabetes) - kisukari hiki kinatokea wakati wa ujauzito na hupotea baada ya kujifungua mtoto.
- Shinikizo la damu (hypertension)
- Shinikizo la damu wakati wa ujauzito pamoja na kifafa cha mimba (pre-eclampsia & eclampsia)
- Kuzaa kwa njia ya upasuaji (caesarean section)
- Tatizo la kiumbe kutopata hewa vizuri wakati wa ujauzito (fetal distress)
Vidokezo Muhimu
It’s all about Exercise, Diet and Discipline in shredding weight not Expected Due Date/ Expected Date of Delivery as some of you might think.
Today I would like to share my own experience in reducing body weight, in case you are overweight or obese. In November 2010 I was weighing 105kg, and my BMI indicated ‘obese’. Well, I could easily get tired, sometimes could not walk fast, yet I continued to play soccer once in a week. The funny thing was, I was a very good preacher to people on weight reduction programs, interventions and other bla bla accompanied to such health talks. Basically I could not walk the talk!
One day I woke up in the morning thinking on the whole issue of body weight reduction. And this was preceded by a talk to a very close friend of mine who later became my motivator. I planned and decided I should reduce weight significantly.
Well, my initial intervention was to reduce food intake and started jogging. That was in November 2010. Normally I used to eat large amount of food and bad enough not paying attention to even caloric foods, sugary drinks like sodas etc. So I significantly reduced this, even the amount of sugar in tea or coffee. I started jogging for about 45minutes in the morning for 6 days in a week. I left one day to rest my body. In a month I managed to reduce the weight for about 5kg. Well some might think that was too much reduction, but I felt fine and motivated.
After two consecutive months, I was weighing 98kg. Then I set up a goal of reducing 2-3kg per month, and the monitoring of weight was done on the same weighing scale at every end of month. I maintained the discipline on what to eat, the frequency and amount. I concentrated mainly on protein-rich foods like fish, chicken (not fried one), beans, vegetable and the likes. I made sure that I have a heavy breakfast knowingly that it would help me providing energy throughout the day and later on during my exercises. During the day, I started having in-between meals in small quantities, yet being cautious and staying away from sugary foods, fried and fat-content foods. Running away from these foods needs courage…imagine the taste, yummy-yummy nature of these foods, it needed and needs highest level of self discipline. Well I even ran away from alcohol as well. As it is well known, alcohol produces sugar in the blood, so I reduced significantly alcohol taking.
After reducing at least 10kg, I started attending the gym, the main goal to reduce weight by burning fats and packing some muscles back. The advantage of gym was that I could use the machines for timed/interval exercise like treadmills. From literature and experience, this type of exercise is good for burning of fats in the body, leaving the lean muscle behind. If you are an experienced jogger, you can tame interval exercise by use of watch to have intervals of sprinting and jogging.
Sprinting makes the heart to pump on high rate thus delivering oxygen to the fat burning process in the body. Reverting the body to jogging state, make the heart to slow down and thus you inhale more oxygen ready for another episode/interval of sprinting. This kind of exercise is advised to be done three times a week as it burns a lot of calories if done correctly.
Well, I have been attending the gym at least on daily basis, not only doing the interval exercises, but also lifting weights. Lifting weights also helps to burn fats and hence pack some muscles.
The effect I have seen in my body so far is that I have reduced the weight significantly meaning that I have to go back to shops and buy new trousers and shirts! My tummy has reduced so much, so is the waist circumference – a good indicator on fat deposits on the body. My goal was to be 85kg six months after weight reduction course and I have achieved that through Exercise, Diet and Discipline to those two! My take is weight reduction is possible and needs one to have a discipline in order to achieve the goal. The goal is normally like a mathematical equation with factors relying on exercise, diet and discipline. When one of the factors is not appreciated, the goal cannot be achieved and it becomes easy to go back to the state you were in initially..overweight, obese and the likes!
Na Issa Kapande
Ni muhimu kwa mzazi/ mlezi kufahamu aina ya chakula kimfaacho mtoto wake hususani yule aliye katika umri wa miezi tisa na nusu mpaka miaka sita. Aina hizi za vyakula na jinsi ya uandaaji wake hutofautiana sana na zile anazokula mtoto mkubwa au mtu mzima. Leo, mtaalamu wetu wa mapishi, Chef Issa anatuletelea ratiba ya chakula cha mtoto wa umri huo.

